Gharama za Kumwozesha Binti

Egypt's Dar Al-Ifta

Gharama za Kumwozesha Binti

Question

Je, gharama za kumwozesha binti na matumizi yake ni wajibu wa nani, baba au mama?

Answer

Kwa jina la Mwenyezi Mungu, sifa njema zote ni za Mwenyezi Mungu, na rehma na amani zimwendee bwana wetu Mtume wa Mwenyezi Mungu, jamaa zake, Maswahaba wake na wanaomfuata. Na baada ya hayo:

Hakuna tofauti kati ya Wanazuoni wa Fiqhi kwamba matunzo ya watoto wadogo – wawe wa kiume au wa kike – ni wajibu kwa baba zao. Imamu Al-Mawardi alisema: "Matunzo ya watoto ni jukumu la baba zao, kwa ushahidi wa Kitabu (Qur’ani Tukufu), Sunna, Ijma’a na maelekezo ya kisharia." Ama kutoka katika Kitabu (Qur’ani Tukufu): Ni kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu: {Na juu ya mwenye mtoto ni kuwaruzuku na kuwavisha kwa wema} [Al-Baqara: 233], ambapo aya hii inaonyesha kwamba gharama za watoto ni wajibu kwa baba, si mama” imenukuliwa kwa muhtasari[1].

 

Imamu Al-Qurtubi alisema: "Aya hii ni dalili ya wajibu wa baba kuwahudumia watoto wake kwa sababu ya udhaifu wao na kutoweza kwao. Mwenyezi Mungu alimnasibisha mtoto kwa mama kwa sababu chakula kinamfikia kupitia kwake kupitia kunyonyesha, kama alivyosema: {Na ikiwa ni wanawake wajawazito, basi wagharamieni} [At-Talaaq: 6], kwa kuwa chakula kinamfikia mtoto kupitia mama." Wanazuoni wote wamekubaliana kwamba ni wajibu kwa mtu kutoa matunzo kwa watoto wake wadogo wasiokuwa na mali.
Mtume (S.A.W.) alimwambia Hind bint Utbah, alipomwambia: “Hakika Abu Sufyan ni mtu bakhili, hanipi matunzo yanayotosha mimi na watoto wangu isipokuwa kile ninachokichukua bila yeye kujua. Je, nina hatia kwa hilo?” Mtume Akasema: "Chukua kinachokutosha wewe na watoto wako kwa wema."[2]

Kwa hiyo, Matunzo ya binti ni jukumu la baba, si mama. Baba anawajibika kutoa mahitaji yote muhimu kwa watoto wake kama chakula, mavazi, na mengineyo kwa mujibu wa desturi ya jamii na hali ya kifedha ya mtu kama yeye.

Na Mwenyezi Mungu Mtukufu ni Mjuzi Zaidi

 

[1] Alhawy, 11/447, chapa ya Darul-Kutub Al-Ilmiya.

[2] Al-Jami’I liahkam Al-Quran, 3/163, chapa ya Dar A’alam Al-Kutub.

Share this:

Related Fatwas