Swalah ya Al-Fjiri kwa wanaosafiri kabla yake.
Question
Jinsi ya kuswali Swala ya Al-Fjiri kwa wale wanaosafiri kabla yake?
Answer
Muislamu akianza kusafiri kwenda sehemu yake ya kazi kabla ya Adhana ya Al-Fajiri kisha muda wa Swala ya Faradhi ukaanza: Ikiwa anajua kwa ada kuwa atafika anapokwenda na akaweza kuswali, hali ya kutimiza masharti na nguzo za Swala kabla ya jua kuchomoza; basi aicheleweshe mpaka wakati huo. Na ikiwa atajua kuwa hatafikia chochote katika haya mpaka baada ya kuchomoza jua, na haiwezekani kwake kuswali kwa ukamilifu wa masharti na nguzo za usafiri; aiswali hapo kwa kutimiza masharti na nguzo anazoweza kuzifanya, na baada ya hapo inapendeza arudie Swala ikiwa muda wake umebaki, au ailipe ikiwa muda umeisha.
Arabic
Englsh
French
Deutsch
Urdu
Pashto
Hausa
